Ijumaa, 26 Juni 2015

FAIDA ZA TENDE



FAIDA ZA TENDE NA MAJI WAKATI WA KUFUNGUA

 TENDE imesifiwa saana na mjuzi wa  elimu kua ni tunda miongoni mwa matunda bora na hakika alisemalo MTUME MUHHAMAD REHEMA NA AMAN ZIWE JUU YAKE ni vyema kuliangalia mara mbili kwan asemalo kwa kukataza au kutusisitizia kuliendea hua kwa mwanadamu yoyote ni bora kwake kuliko tunavyo fikiria.
© tibazakissuna.blogspot.com
VILIVYOMO NDANI YA TENDE

Energy282 Kcal
Proteins2.5 g
Fiber8 g
Fat0.4 g
Folate19 mu gs
Iron1.09 mg
Vitamin K2.7 mu g
Magnesium43 mg
Potassium656 mg
  
MARADHI YA MOYO ::
                     tende husaidia moyo na mishipa kwa kua hufyonza cholestrol katika mishipa na FIBER hujulikana kwa kusaidia moyo , Hivyo hua na msaada kwa watu wanao ugua shinikizo la damu

© tibazakissuna.blogspot.com


KUPUNGUZA UZITO ::
                    tende hua na tabia ya kushibisha upesi kutokana na wingi wa fiber ambayo huleta nguvu na mwili kuwa na maridhio ya kiwango cha chakula kilichopo tumboni

 KUSAIDIA MMENGENYO ::
        tende tunda lenye fiber nyingi ambapo husaidia mmengenyo wa chakula kwa kusafisha (gastrointestinal system) na kuupa mwili nguvu  

HUSAIDIA AFYA KWA MJAMZITO NA MWANAE  ::
kwa mjamzito kula tende kuna faida zaid ya nane kwake yeye na mwanae haswa kuimarisha afya zao na pia ni msaada mkubwa kwa mwanamke anaetaka kujufungua husaidia kujifungua bila misukosuko ya njia na uchungu

HUIMARISHA MIFUPA ::
               Tende pia hua na calcium ambayo huimarisha mifupa na kutibu maradhi ya mifupa na maumivu (arthritis)


HUIMARISHA UBONGO ::
                  Utafit ulio fanyika (JAMA INTERNAL MEDICINE) inaonyesha kua ubongo huimarika na kufanyana kufanya kazi vyema kwa akili kutokana na VITAMIN B6


HUONGEZA NGUVU ZA KIKE NA ZA KIUME ::
  Changanya tende  maziwa na asali jaribu alafu utanipa jibu lake


TIBA YA KUHARISHA ::
    hutibu kuharisha kama utachanganya na asali

HUONDOSHA MALARIA ::
    Kula chembe saba baada ya Salat alfajri pamoja na maji ya vugu vugu kikombe kimoja

MTUME MUHAMADI REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE ALIKUA AKIPENDA KULA TENDE NA KUTUHUSIA KUFUNGUA KWA TENDE 

© tibazakissuna.blogspot.com


>> KWANN UFUNGULIE MAJI YA MOTO NA SIO YA BARIDI NA SODA

a) unapo kua umefungulia maji ya moto husaidia kuyeyusha mafuta mafuta ndani ya mwili 

b) maji ya moto husaidia kuyeyusha chakula na kufanya mmengenyo ufanyike kwa wepesi na uchafu kutoka kwa wepesi

c) husaidia ngozi kupuumua kutoa jasho na kuondoa mafuta futa na kufanya upumuaji mzur na kujiskia upo vyema 

d) huondoa uteute ambapo uteute husaidia kushika wadudu na kuowaangamiza hivyo unapo kunywa maji ya moto hufungua njia ya koo na pua na kukusaidia koromea kushusha uteute utaoenda kutolewa kama uchafu

e) unapo kunywa maji ya moto mwili hupandisha joto na kukusaidia kuondoa uchafu kwa njia ya jasho

© tibazakissuna.blogspot.com

KWANIN USITUMIE MAJI YA BARIDI

1) Maji ya baridi hufanya mfumo wako wa mmengenyo kufanya kwa tabu kwani mwili utapoteza nguvu zake kuhakikisha maji yamekua ya moto nguvu hiyo huenda ingetumika katika kumengenya chakula ulicho kula

2) maji ya baridi hufanya mafuta kuganda hivyo kama ulikua na sababu ya kupungua uzito zoezi litakua gumu 

3) huatarisha kushindwa kufanya kazi kwa figo

4) soda zina madhara mengi ikiwa utaanza kufungulia soda una nafasi kubwa ya kufyonza sumu yake vyema 

© tibazakissuna.blogspot.com
 
FAIDA KWA ALIE FUNGULIA TENDE

1) tende huzuia kiungulia na pia husaidia mmengenyo wa vyakula hivyo mtu anae futuru hua ni funguo inayo saidia vyakula utavyo kula

2) tunajua tende husaidia kupunguza kasi ya kula haswa ukifungulia hua ni sababu ya kukusaidia kuto kula saana na kufanya afya yako kuzid kuimarika

3) husafisha mwili kutokana na magonjwa na kuupa mwili nguvu 
© tibazakissuna.blogspot.com

IKIWA MUDA UTAPATIKANA TUTAELEZEA FAIDA ZA TENDE KWA MAMA MJAMZITO


Ijumaa, 19 Juni 2015

FUNGA




FAIDA ZA FUNGA 

MTUME MUHHAMADI  rehema na amani ziwe juu yake amesema :: FUNGENI MPATE AFYA

pindi unapo kula chakula mfumo wa mmengenyo wa chakula huvunja vunja CARBOHYDRATE  kuwa katika GLUCOSE(sukari) kwa ajili ya kuupa nguvu mwili hivyo glucose hufyonzwa kutoka katika njia za mmengenyo na kupelekwa katika damu kisha huenda mpaka kwenye cell hapo INSULINI sasa hufungua SELLI za mwili kuingiza sukari hitajika

sasa usipo kula mwili hupungukiwa na glucose katika damu na hapo huanza kutafuta stoo (store) ya mwili inayo itwa GLYCOGEN na gylcogen inapo ishiwa basi huchoma mafuta na misuli iliyo ongezeka ili kuupa mwili nguvu.
  kwa hiyo kutokana na hayo maelezo hapo juu utajua zaid faida ya kufunga kama ifaatavyo

© tibazakissuna.blogspot.com

1) HUTIBU MARADHI YA MOYO
mafuta hua ni sababu nzur ya moyo kuto kusukuma damu ipasavyo na kuufanya moyo kufanya kaz mara mbili zaidi ili kusukuma damu ifike shemu husika sasa unapo funga na ukawa unajishughulisha na kaz za kawaida lazima mafuta hayo yaondoke mwili

2) HUPUNGUZA UZITO 

 Kwa watu walio wanene na wenye vitambi hii ina maana kua GLYCOGEN (stoo ya chakula katika  mwili ) ni kubwa hivyo unapo funga glycogen zenu zitatumika ipasavyo na kufanya mwili kupungua na kukusaidia kupandisha kinga asili ya mwili kwan acid inatoka

3) HUTIBU KISUKARI TYPE 2

katika ugonjwa huu selli za mwilim hua sio sikivu kwa insulini (kidhibiti cha glucose katika damu)  hivyo mtu akifunga insulini hua na nguvu (sensitive) ya kutuma signal  kuiambia (GLUCOSE KISAFIRISHI) kusafirisha glucose katika seli  kwani ugonjwa huu hutokea pale SIGNAL hiyo inapo zuiwa na kusababisha selli kuto chukua sukari hiyo hivyo hulepelekea sukar kuwa juu

4) HUTIBU KIHARUSI NA MISTUKO

Unapo funga mfumo wako wa moyo na mishipa (cardiovascular) hufanya kazi vyema na kutibia magonjwa yalio katika mfumo huo sasa kama tunavyojua kama  mfumo wako wa damu utafanya kazi vyema inamaana uwezo wa ubongo kupata oxygen ya kutosha utakuepo hivyo ubongo utafanya kazi ipasavyo

5) HUPUMZISHA MMENGENYO

Maradhi mengi hukulia na kukomaa katika mfumo wa mmengenyo na kisha husambaa kwenye damu pindi mmengenyo unapo kua umepumzika hali ya vijidudu vinavyo leta maradhi hufaa na mwili kujisafisha kupitia metabolism

6) HUONGEZA UMRI

ni kweli kua kula bila kushibisha tumbo hukuongezea umri wa afya njema katika maisha hivyo ubora wa kufunga ni mara mbili yake kwan maradhi meng yanatokana na kula ovyo ambapo hufanya asid kua juu na magonjwa hatar kama microbes kustawi

7) HUKUZA UWEZO WA UBONGO (akili)

kufunga imethibitishwa kuongeza uwezo wa ubongo kwani husaidia kuzalishwa kwa protein inayoitwa ( brain-derived neurotrophic factor (BDNF.)} kutoka 50 mpaka 400 ambayo husaidia kulinda ubongo kutokana na mabadiliko na pia kuzalisha neurons

© tibazakissuna.blogspot.com

 8) HUTIBU NGOZI NA CHUNUSI

kwakua mwili unapata pumziko la kusaga na kusambaza chakula basi huamishia nguvu zake katika kujenga mwili na kuuboresha haswa kuanzia kwenye ngozi 

9) HUKUTIBUA ASTHMA NA MATATIZO YA USINGIZI

funga huweza kuonda tatizo hili kwa kupunguza chumvi na maji mwilini na pia hupunguza uvimbe wa tissue hali inayo weza msaidia mtu kulala vyema na kuondosha shida ya kupumua

10) HUTIBU NAFSI

#TABIA huanza kama uamuzi kisha hua Tabia ambapo hukua na kua mraibu/teja (addicted)  na utajua kua upo addicted pindi unapo taka kuliacha jambo hilo na kushindwa hapo jua upo katika hali ya addiction
Allah mjuzi zaidi ila ili kuibadilisha tabia ya mtu huchukua masiku 30

hivyo REHAB ( sehemu za kurekebisha tabia ) hua ni siku 30 na WAISLAM tunafunga siku 29 mpaka 30
hivyo miongoni mwetu tuna ingia kufunga ili kutibu maradhi yaliyo ingia katika nafsi mfano 

KUVUTA SIGARA BANGI NA UNYWAJI POMBE

KUJICHUA > njia hii hua ni njia bora zaid ya kujikinga kwani mfumo wa divide and conquer huingia vyema katika swala la funga na kukusaidia kumiliki matamanio yako na kujihifadhi

UZINIFU >  mwenzi huu ni mwenz wa kujihifadhi kwanzia macho mpaka utendaji na ukifunga matamanio hupungua kwa kiasi kikubwa wanasayansi wamethibitisha hili kua njia nyepes na yenye kusaidia bila madhara

KUTOKUSWALI wengi wetu tumekua tukikwepa kuswali ila mara nying ndan ya mwenz huu weng wetu tunajitahid kuswali sio jambo linalo pendeza kuwasema watu wanajitahid kurud kuswal au kuwakatisha tamaa kua wanaswal kipind flan mpaka kipind flan kikubwa tupeane moyo ili kumsaidia mtu huyu swala imuingie katika tabia yake na iwe ni sehemu ya maisha yake ya kila siku kwan FUNGA ni sehemu ya kurekebisha na kumpa mtu afya ya nafsi na mwili

KUSENGENYA NA KUTUKANA > mwenzi huu hukupa haya na aibu ya kufikiria mara mbili jambo kabla hujaliendea jambo hivyo hukufunza aibu ukiwa na AIBU UNAKUA NA ADABU


HIVYO KUA MKWELI KWA SWAUMU YAKO ISHIKE NAFSI YAKO NA UTAPONA KWA UWEZO WA ALLAH MARADHI YA NAFSI NDANI YA MASIKU 29 MPAKA 30

© tibazakissuna.blogspot.com