Jumatano, 31 Desemba 2014

MTU ANAYE PANDISHA MAJINI ANATOA MAJINI?


Hili ni miongoni mwa jambo ambalo watu wengi wamekuwa wakipata SHIDA KULIJUA na kujikuta wakipoteza muda na gharama ili kupata tiba,
Matokeo ni shida kuzidi badala ya kupungua.

 Leo hii wanaadamu wengi tumekuwa na kasumba mtu mwenye kupandisha MASHETANI ndiye TABIBU MZURI, na husifiwa kwamba ni mtaalamu, ila walisha sahau nini?

UPELEKA MGONJWA WAKO KWAKE ILI ATIBIWE KWA SABABU ANAPANDISHA MASHETANI, matokeo unafika kwa mganga bingwa ukiwa umemkuta na yeye KAPANDISHA MASHETANI VILEVILE.  kweli kuna tiba hapa?

amini ukweli ni kwamba wamekutana WAGONJWA WAWILI. wenye kusumbuliwa na ugonjwa mmoja, na wote wanahitaji kutibiwa ili waachiwe na mashetani.
Suala la mwanaaadamu kupandisha mashetani usije kufikiri kwamba ni ujanja wala si ucha Mungu. ila shida na hasara kwa sababu
26:221 QUR AAN
 Allah anataja sifa ya wenye kushukiwa na mashetani
usije ukapotea muda kuhangaikia TIBA kumbe wewe  umekutanisha wagonjwa wawili chumba kimoja matokeo ni kelele na nyimbo tu.
 HUWEZI  KUTOA JINI  UKIWA UMEPANDISHA JINI
tibazakissuna.blogspot.com

DUAA NI KINGA YA MUUMINI


Jumanne, 30 Desemba 2014

UTAMJUAJE JINI ANAYE KUTESA?


MAJINI NA UTAMBULISHO WAO (HOW TO IDENTIFY THE EVIL SPIRIT THAT POSSESSING YOU)

Kujua aina ya JINI anaye kutesa, huwa inaambatana sana na mfumo wako wa maisha yako kwa ujumla. haswa kwa njia ya :

1) mavazi

2) ndoto

3) tabia

mifumo hii inatosha sana kukujulisha aina ya jini akusumbuaye na jinsi ya kukaa naye mbali.


MFANO

1) unapolala na kuota wanakuja watu wamevaa NGUO za NJANO
basi angalia tabia yako itakayo kuandama, 
utakuwa mwenye kupenda KULALA unapokuwa msikitini hasa wakati wa khutba.
pia utakuwa huelewani na waislam bali utakuta wengi rafiki zako ni wakristo, 
utakuwa ukipenda kuongea kiingereza hata kama hukusoma na huna elimu. nandoto za kuota safari ya ulaya ima kukaa na wazungu 


TIBA
hawa wasilimishwe kisha watolewe


2) kuota watu wenye NGUO za BLUU SAMAWATI,
 humaaanisha kwamba una majini wayahudi, na tabia yako ni kuwa mnafiki na mgombanishi, huwapendi waislam wala wakristo. unakuwa hupatani na maongezi ya dini.lakini pia ibada hufanyi. wewe ni uongo na kupenda madaraka. hawa MAJINI WAYAHUDI 
hawa wakipanda hujifanya waislam, au wanadai wao ni walinzi. ni


TIBA
wakuwaondoa ima kuwaua


3) kuota watu wamevaa NGUO NYEUPE
basi itakupelekea kuwa mpole mpaka kero, pia utakuwa na huruma kupita kiasi, halafu una mapenzi na huruma kwa waislam, majini hao ni waislam. lakini hawaujui uislam, 

TIBA
wakilinganiwa hutoka bila tabu


4) kuota watu wenye NGUO NYEUSI 
basi itaaambatana kuwa mwenye kupenda ngoma na historia za kale,
unapenda simulizi sana, mvivu wa ibada.  
sababu MAJINI HAO NI WAPAGANI
tibazakissuna.blogspot,com


TIBA
inakubidi uwasilimishe na kuwatoa

kumbuka majini ni wakaidi na watukutu sana, huwa akikubali kutoka kirahisi basi huwa anaendelea kufanya hila ya kutaka kurudi tena mwili na visa ndani ya miezi mitatu siku 90. 
kumkomesha kwake ni tibazakissuna.blogspot.com

upate MAFUTA YA  ZAYT SHIFAA ,
ambao ni mchanganyo wa mafuta maalum kisha upakae kwa siku 90
na basi utakuwa umewakomesha vyema majini AINA ZOTE.

pia usisahau KISOMO
kisomo ni muhimu sana ili dawa iwe ni yenye kufanya kazi.

USIKOSE kuwa unatembele hapa kwa elimu zaidi
tibazakissuna.blogspot.com

Jumapili, 28 Desemba 2014

TIBA YA SIKIO


Ndugu yangu jinusuru na UZIWI kwa kutumia tiba nyepesi isiyo na gharama. kwanini uzaliwe kamili kisha uruhusu uziwi?
Hakuna ugonjwa usio na dawa, haya maneno kasema MTUME MUHAMMAD SAW   na ndiyo mana tupo kwa ajili ya kuthamini maneno haya.
iwapo sikio linauma au kutoa usaha
basi wahi kuondoa tatizo hili kwa kutumia

 1) mafuta ya habat sauda

 2) mafuta ya vitunguu thaum

 3) mafuta ya kenge

JINSI YA KUTUMIA

tibazakissuna.blogspot.com
mafuta ya habat sauda ml 20

mafuta ya vitunguu thaum ml 20

mafuta ya kenge ml 50

kisha changanya pamoja,halafu weka TONE KIDOGO katika sikio linalo tatiza kisha weka pamba ulale.

Utatumia kwa SIKU 19 . kisha baada ya hapo utakuwa salaama in shaa Allah
na ukisha tumia na kupata majibu mazuri usisite kutujulisha kwa mafundisho yetu mazuri ya  tibazakissuna.blogspot.com

TIBA YA MENO


TIBA YA MENO (TEETH INFECTION)

Kwakweli meno ni kitu kidogo ila thamani yake ni kubwa sana.
Leo imezuka msemo kuwa dawa ya jino ni kung'oa, sasa hebu jiulize hivi unatang'oa meno mangapi kama si kutafuta kuwa kibogoyo?
kama dawa ya jino kutoa,kwanini dawa ya kichwa isiwe kukikata?
huu ni msemo mbovu kwa sababu msemaji hakuwa akijua zaidi juu ya meno.
nusuru meno yako kwa 
tibazakissuna.blogspot.com

NUNUA DAWA ZIFUATAZO

1) SHABU

2) KARAFUU

3) MDAA

dawa hizi hakikisha umesaga na kuupata unga wake kisha uuchanganye vyema.  
Ukiisha kuuchanganya kifuatacho ni namna ya kutumia.

MATUMIZI

chota dawa KIDOGO SANA kisha weka katika mswaki,halafu uwe unaswaki kwa dawa hii bila dawa nyingine.

KWA JINO LILIOTOBOKA

chukua dawa kidogo kisha weka katika PANGO LA JINO na ufumbe kwa dakika 5
halafu sukutua na kutema kisha weka nyingine katika mswaki
utafanya hivyo ASUBUHI NA USIKU 
mafanikio utakayo yapata kwa kuimarika meno yako basi usione shida kutupa TAARIFA kwa tibazakissuna.blogspot.com

Alhamisi, 25 Desemba 2014

DAWA YA HOMA YA MATUMBO



HOMA YA MATUMBO (TYPHOID FEVER) 

ni maradhi mabaya tena yanakosesha raha na amani popote unapokuwa kutokana na adhabu inayokuwepo tumboni mwa mwenye kuumwa.

SABABU LA TATIZO HILI

  • Utumiaji vyakula visivyo vya moto au vilivyo poa kwa lugha nyepesi, 

  • Unywaji wa maji yasiyo salama, 

  • Kula kwa mikono michafu. 

Sababu ni nyingi kwa kweli.
 © tibazakissuna.blogspot.com
lakini pia ugonjwa huu ni wenye kutibika kwa haraka iwapo utatumia njia ya kujitibu kisuna, na kufuata maelekezo kamili.

DAWA ZA KUTUMIA

1) HULBA YA UNGA [uwatu]

2) SANAMAKI YA UNGA.

tibazakissuna.blogspot.com
kisha changanya vyema halafu ukisha changanya utakuwa unachota ujazo wa kijiko kikubwa kimoja na kuweka katika uji mwepesi usio na sukari na kisha unywe asubuhi na jioni kwa siku 9. utapona kabisa in shaa Allah
tibazakissuna.blogspot.com

Jumatano, 24 Desemba 2014

JINI UMMU MULDAMI ANAVYO SABABISHA UVIMBE KATIKA KIZAZI.

 

 UMMU MULDAMI (EVIL SPIRIT/DJINN)

Ukiongea kuhusu jini aina hii aitwaye UMMU MULDAMI, jua kwamba unaongelea jini M^BAYA miongoni mwa MAJINI WAKOROFI.
Jini huyu huwa anakaa katika MFUKO WA KIZAZI na kutumia aina ya uchawi uitwao AQUMI.Kisha uchawi huo hukaa katika MIRIJA YA UZAZI na kusababisha UVIMBE katika kizazi.
Jini huwa ni hatari na ni msumbufu sana.
tibazakisunna.blogspot.com
Jini ummu muldami husababisha maradhi mengi katika mwili wa binaadamu,

DALILI ZA KUKUJULISHA UNA JINI UMMU MULDAMI

1) kushikwa ngiri wakati wa joto

 2) kushikwa chango linalo zuia mkojo

 3) mwanamke kukosa hedhi miezi mitatu hadi nane mfuatano

 4) mwanaume kuwahi kushusha manii haraka

 5) mwanaume kusinyaa uume wakati wa jimai katikati ya tendo

 6) mwanamke kuwa na maziwa kama mjamzito

tibazakisunna.blogspot.com
Jini huyu pia ni mgumu kupanda ila husababisha MAUMIVU MAKALI YA KICHWA maeneo ya KICHOGONI.kisha kujikuta midomo ikitetema na kushindwa kuongea.
lakini kwa neema ya Mola kuna njia ambayo ukitumia huondoka kisha mtu akapata mtoto,lakini bila kumuondoa huwa ni ngumu sana kwa wanandoa kupata mtoto.
tiba yake inakubidi upate mtu mwenye kujua na Ucha Mungu.ili afanye kisomo kwa muhusika.
aina ya dawa kwa mgonjwa huyu ni

1) sanamaki

 2) zattari

 3) hulba

 4) sufa

 5) khardal
tibazakisunna.blogspot.com


CHANGANYA ikiwa zote ni UNGA na upate kiasi cha gm 200
na kunywa katika uji wa MTAMA au ULEZI usiwekwa na kitu chochote zaidi ya sukari hafifu. siku 30. huku akifanyiwa kisomo cha yaasin saaqitw siku saba
in shaa Allah atakuwa mwenye kupona. na pia usisahau kumpa mafuta ya kupakaa kwa siku 30 ambayo ni ZAYT SHIFAA ili kumuua nguvu JINI.
tibazakisunna.blogspot.com

Jumanne, 23 Desemba 2014

WAJUA KUWA MAJINI NA WACHAWI HUUGOPA MKUNAZI !!!!

MKUNAZI NA UCHAWI ( JUJUBE TREE REPEL SPIRIT AND WITCH )


Amini ndg yangu, unapoongelea mti wa MKUNAZI basi unaongelea ule mti ambao Allah ameuita SIDRAT L MUNTAHA, yaani mti unao maliza mambo yote, au mwisho wa mambo,
WAKRISTO wakauita mti wa uzima, japo mkiristo hajui mti wa uzima ni mti gani, ila kwa taarifa mti huo ni MKUNAZI.

KWANIN MAJINI NA WACHAWI HAWAPEND MTI HUU ?


mti huu huwa unapendwa sana kukaliwa na malaika wakubwa kama RAUQAYAAIL,SAMSAMAAIL,GHANAAIL,ISRAHAMAAIL,DARDAAIL nk.
hivyo majini wote waasi na wachawi huwa wanapofika mahali penye mti wa mkunazi hawawezi kukaa wala kusimama mahala hapo.
na ndiyo maana mkunazi unapo kuwepo basi katika nyumba hiyo huwa hafiki mchawiwala shetani.  tibazakisunna.blogspot.com

FAIDA YA MKUNAZI  

tibazakissuna.blogspot.com
mkunazi una faida nyingi sana

1) majani yake ukiloweka na kuogea iwapo utasomea aya za qur aan basi utaepukwa na kukaliwa mbali majini aina 10 wakorofi ambao ni

1) jalwush,

2) ummu muldami 

3) ankis 

4) ghaughaan 

5) bedui bidwaan 

6) makata wa makatani

7) maymuna l hind'

9) zawaabil 

10) atruush

majini hao kamwe hawata mdhuru tena mtu iwapo atafanyia kisomo maalum cha KHAWAATIMU katika maji yaliyo lowekwa majani ya mkunazi.
pia majani ya mkunazi iwapi unaumwa KIFUA SUGU lakini si pumu, chemsha pamoja na ndimu kisha unywe kwa siku 14 utapona, 
 kama UNAWANGIWA au kutembelewa na wachawi mara kwa mara basi chukua MAJANI YA MKUNAZI kisha weka HAIJALI na FAYJALI loweka pamoja na usomee kisomo cha KHAWAATIMU, kisha umwage ndani ya nyumba au shamba na wachawi hawatokujia tena kukudhuru. ndg mkunazi una mambo mengi sana ambapo ukiwa nao unaweza kufungua clinick kwa kutumia majani ya mkunazi tu.  tibazakissuna.blogspot.com

Tabia ya mti huu ni ajabu sana kama ulivyo mti wa MZAYTUNI,mtu mwenye roho mbaya akipanda basi mti huu hauoti

na mchawi akipita katika eneo lenye mti huo, basi ajue mtukuta asubuhi, na HATOONDOKA mpaka wachawi wenzake waje wamlipishe faini, na vipi utamgundua mchawi aliye naswa katika nyumba iliyo fanyiwa kisomo cha khawaatimu kwa majani ya mkunazi?. utamkuta akiwa katika umbo la paka mweusi au nyoka aina ya cobra
 unapo hitaji kujua zaidi basi tembelea blog yangu tibazakissuna.blogspot.com
utapata mengi.


Alhamisi, 18 Desemba 2014

KWANINI MAJINI WANATESA BINAADAMU?


MAJINI KUTESA WANADAMU (SPIRIT VENGEANGE)

Sababu ya ugomvi wa Binaadamu na Jini ni ugomvi wa madaraka,
QUR 761
mwanaadamu ni kiumbe wa mwisho kuletwa hapa duniani lakini kaja na kuwa KHALIFA,
Wakati wao majini walikuwepo kabla ya Mwanadam kisha wamekuwa WATAWALIWA, hili ni jambo ambalo majini wamelijengea CHUKI kiasi kwamba mwanadamu anapoishi nje ya sheria ya uislam huwa mwepesi sana kuingiwa na kudhurika kutoka na majini.
 © tibazakissuna.blogspot.com

MAJINI HUINGIJAE KWA MWANADAMU?

majini huingia kwa mwanaadamu kupitia tundu zilizopo katika mwili wake, na wanapita katika MISHIPA YA DAMU na kukaa katika MOYO  au UBONGO wa nyuma medula oblangata.

MIFUMO GANI HUTUMIKA KUMDHURU MWANADAMU??

mifumo ambayo jini anatumia kumumuumizia mwanadamu ni mitatu, ambayo ni mifumo ya kichawi.

1) KHOFU

2) USINGIZI

3) CHAKULA.

hii milango mitatu ambayo wachawi na majini huitumia kumuumizia mwanadamu, tibazakissuna.blogspot.com
mila ngo hii muwa inamuumiza vipi mwanadamu

1) mtu muoga huwa anaingiwa haraka na majini na ni mwepesi kurogeka

 2) mtu mwenye kulala lala hovyo rahisi kurogeka pia rahisi kuingiwa na majini

 3) mtu mlafi anarogeka haraka na rahisi kuingiwa na majini.

kama utajilinda na mifumo hii ambayo imetajwa basi ni vigumu kurogeka au kuingiwa  na majini.
tibazakissuna.blogspot.com


MAJINI NI KINA NANI???

JUA KUHUSU MAJINI (WHO ARE SPIRIT/DJINN)

MAJINI na viumbe katika viumbe vya ALLAH na wameletwa duniani ili wamuabudu aliye waumba
51:56 qur aan
lakini viumbe hawa Majini wamekuwa wakisumbua sana binadamu na kuwatia maradhi ya kila aina, kwa nini majini wawatie maradhi na kusumbua wanadamu?
kuna tofauti baina ya mwanadam na jini katika maumbile yao. suurat Rahman,
majini wameumbwa kwa UPEPO WA MOTO na wanaadamu tumeumbwa kutokana na UDONGO.
lakini majini hawatupendi sana binadamu japo kuwa sote tumeumbwa na Allah.

       NINI MAANA YA JINI??

© tibazakissuna.blogspot.com
jini ni kiumbe ambaye amefichwa kuonekana kwa macho ya kibinaadamu, na ndiyo maana wakaitwa majini kwa sababu ya kuto onekana na macho ya binaadamu.
na majini waliomba kwa Allah mambo matatu baada ya kufa nabii Suleyman bin Daud as.
walichoomba

1) waishi umri mrefu

2) wawe wanabadilika kuwa kiumbe watakacho

3) wasionekane na binaadamu,

 Allah kawakubalia kwa kuwapa umri mrefu na wanaishi mpaka miaka 1000.
kisha wanabadilika kuwa kiumbe kungine lakini wanakaa kwa MUDA si umbo la kudumu, wakiamua kubadilika wanabadilika kuwa

1) paka

2) nyoka

3) binaadamu nk

na kuhusu kutoonekana wana jificha kwa wasio na elimu lakini kwa wenye elimu hawajifichi na wanaonekana, ila si kwa umbo halisi.
na majini wamegawika katika makundi 660.
pia majini wapo dini na imani tofauti               
tibazakissuna.blogspot.com 

Jumatano, 17 Desemba 2014

MWILI KUFA GANZI

MWILI KUFA GANZI

Mwili wa binadamu una njia za fahamu ambazo humsaidia mwanadamu kujua na kuhisi nin kinaendelea ndani ya mwili 

tuchukulie mfano wa mtu alie jikwaa kwenye kidole mishipa ya fahamu huchukua ujumbe wa maumivu na kuupandisha kupitia uti wa mgongo mpaka kwenye ubongo na kutafsiri kua kidole gumba kimeumia hivyo chukua tahadhari ya kuto kukitumia ndipo unaona mtu hakanyagii mguu huo kwa muda maana pia ubongo ukishapata taarifa hiyo hupunguza ujaji wa message ya maumivu  ndipo utaona maumivu huanza kupungua na ukaanza kuchechemea

sasa kuumwa na ganzi ni kwamba njia hizo za fahamu zimeathirika kwa sababu ntazozitaja au zimekumbwa na ugonjwa unao ziathiri

SABABU YA TATIZO 

#KUPATA MAJERAHA KWENYE UBONGO kutokana na ajali au chochote kinachoweza athiri ubongo kwa kugongwa

#MAGONJWA YA KISUKARI kiwango cha glucose huathiri mishipa hii ya faham na kuiaribu

#UNYWAJI WA POMBE KWA MDA MREFU

#BAADHI YA MAGONJWA NA PIA UKOSEFU WA VITAMIN B12 AU VITAMIN ZINGINE

#KUATHIRIKA KWA FIGO NA KUA NA SUMU KWA KIWANGO KINGI KWENYE MWILI

tibazakissuna.blogspot.com

#VITENDO VYENYE KUJIRUDIA RUDIA MFANO TAA ZINYE KUWAKA WAKA HASA YA GAME  MIZIKI YA KURUDIA RUDIA KWA MDA MREFU AU WATU WANAO PANGA WENZIE MISTARI KILA SIKU

#UCHAWI AU MAJINI PIA NI SABABU KUBWA YA TATIZO HILI IKIWA INAAMBATANA NA DALILI ZINGINE ZA KUJUA UNA UCHAWI
 
TIBA YAKE
  • SHARBAT
  • MAZIWA
MATUMIZI

© tibazakissuna.blogspot.com
chukua MAZIWA kikombe kimoja yakiwa ya MOTO,halafu weka SHARBAT vijiko VIWILI kila ASUBUHI na USIKU kwa siku 17.

KAMA NI MAJINI AU WACHAWI

SUPU YA NDIMU, kila siku asubuhi kabla ya kula, unachukua ndimu saba bila kukata wala kumenya unachemsha, halafu unachukua maji nusu kikombe unakunywa asubuhi kabla ya kula siku 19
Allah ataleta shifaa
tibazakissuna.blogspot.com

http://tibazakissuna.blogspot.com/2014/12/mwili-kufa-ganzi.html

MARADHI YA VICHOMI NA MIGUU KUWAKA MOTO



MATATIZO YA VICHOMI NA MIGUU KUWAKA MOTO


maradhi haya kwa muangalio wa kawaida ni kichekesho,
lakini maradhi yenye kutesa na adha kubwa kwa mwenye kukumbwa na maradhi hayo'
lakini huwa yanatibika na jinsi ya kutibu inakubidi ufanye kitu kidogo
chukua dawa ifuatayo
tibazakisuna.blogspot.com

1)  mafuta ya ndimu

2) mafuta ya kitunguu thaum

kisha changanya,

halafu uwe unachua kwa nguvu sehemu zenye vichomi au pale penye kuwaka moto katika mwili wako. fanya hivyo asubuhi na usiku kwa siku 11. utapona kabisa
tibazakissuna.blogspot.com

Jumatatu, 15 Desemba 2014

JINI MAKATA



JINI  MAKATA (EVIL SPIRIT/DJINN)

naye ni miongoni mwa majini wenye hila na shida sana.
jini huyu ni miongoni mwa majini ambao husababisha mtu kuonekana kama hasikii vema,
Pia husababisha tatizo la

1) presha ya kushuka

2) kuanguka kifafa, ila kuanguka kwake tofauti anavyo anguka jini maiti.

makata hupenda kuwa na tabia ya VITISHO na kelele ya kuumiza masikio.
pia hupenda kujifanya MPIGA RAMLI na kutaja siri ya watu.
ni jini muhuni sana.
na akiwa amekuja kishari utamjua kwa kuangukia NYUMA na kuburuzika kimgongo mgongo, huwa hatembei KITUMBO TUMBO, akija kwa maigizo ya amani utaona anakuangalia kwa macho makali na haongei ila midomo inamtetema tuu.
jini huyu ni mtesaji sana kwani hunyonya sana damu mpaka unaweza kuta mtu anakonda na hospital haonekani ugonjwa.
nini ufanye ili kumtoa!!!

  1) inabidi upate fusho chafu

  2) upate na mafuta ya ufuta
 © tibazakissuna.blogspot.com
  3) mafuta ya tini

  4) mafuta ya raihan

  5) mafuta ya thaum

  6) na mafuta ya huut {nyangumi}

changanya uwe unapakaa siku 29

kisomo DUAAU JIBRIL na  KHAWAATIM siku 7

in shaa Allah mola atamponya mgonjwa
na ukiwa na jini mahaba aina ya MAKATA utashangaa jambo moja
mwanamke hushuka mapigo ima ikawa anazimia pindi unapo muingilia, pia unaweza kukuta uume hausimami au kusinyaa ghafla na kushindwa kuendelea na tendo nk
tibazakissuna.blogspot.com

Jumapili, 14 Desemba 2014

MJUE JINI MAHABA NA DALILI YAKE



NI NANI JINI MAHABA (AASHIQ DJINN )


unapoongelea juu ya jini mahaba basi unaongelea jambo muhimu na gumu, kwani majini wapo aina karibia 660, na kila jamii ina kuwa na mifumo yake pindi awapo mahaba.
jini mahaba si jini maalum kusema huyu ni mahaba,
mfano sisi binaadamu hatuna kabila maalumu kwamba hawa ni watu tabia mbaya, ila tabia mbaya huwa kwa mtu mwenyewe ni kwa kabila.
pia jini mahaba si jini maalum kuwa huyu ni mahaba ila majini wote waoi wahuni miongoni mwao ambao husumbua maisha ya wanadamu.

DALILI ZA KUJUA UNA JINI MAHABA

tibazakissuna.blogspot.com
1) Kuwa na hasira zisio na sababu

2) kutokuwa hamu ya jimai

3) kupata maumivu na na michubuko katika jimai

4) kuchoka sana wakati wa jimai.

5) kumchukia mwenza wako pindi anapo kuwa karibu na wewe.
 huyu ni JINI SUBIANI.

6)  kukosa hedhi

7)  kupata hedhi kwa miezi miwili hadi mitatu

8)  kuumwa chango au ngiri mara kwa mara

9)  kushindwa kumwaga manii ufanyapo jimai

10) kuingia na kumwaga manii haraka sana
huyu ni jinni UMMU MULDAMI.

11)  kupoteza ladha ya jimai katikati ya tendo

12)  kuishiwa nguvu haraka

13)  kupatwa maumivu makali ya tumbo wakati ukifanya jimai

14) Kuto kuona ladha yeyote na mwanamke kushindwa kutoa ute na kumpa maumivu
huyu ni JINI JALWUSH
                                    tibazakissuna.blogspot.com
15)  Kuto kubeba mimba

16) Kujaa maziwa kama mjamzito
huyu ni UMMU SUBIANI

 17)  Kuota Unapaa

18)  Kuharibika Mimba kaabla ya Miezi Minne

19) Chunus zisizo SIKIA DAWA

20)  Kuchukia kutongozwa na kuto hitaji ndoa
huyu ni JINI TWAYR {qarnail}

21) Kuto tosheka na jimai
huyu ni MAYMUNA

22)  Mtoto kumuogopa mama yake

23) Kuota unafanya mapenzi

24)  Mama kuto toa maziwa akijifungua

25)  Mtoto kupatwa degedege.
huyu ni MAKATA WA MAKATANI.

dalili ni nyingi kulingana na aina ya jini anaye kusumbua.
tibazakissuna.blogspot.com
tafadhali fatilia mada ndani ya blog yangu ili ujifunze mengi
 

Jumamosi, 13 Desemba 2014

JINI AINA JABALI


JINI JABALI


Tunapo muongelea Jini huyu, tunaongelea jini MKOROFI na mwenye vituko vya uhuni sana.
Jini aina ya Jabali ni Jini ambaye huishi  bara na baharini. na huwa anasumbua sana matabibu pale wanapokuwa hawajamgundua kuwa ni jini jabali.
utamjuaje mtu mwenye jini jabali

DALILI ZAKE

 1) humfanya mtu awe KIBRI sana

 2) mtu huwa anapenda sana UKUBWA

 3) humfanya mtu awe na NGUVU YA AJABU kuliko umri wake

 4) mtu huwa ANAJIAMINI sana.

UPANDE WA NDOTO

1) kuota mtu yupo porini anaelekezwa dawa

2) kuota upo mapangoni

3) kuota upo vitani

4) kuota upo katika majabali ndani ya bahari

5) kuota upo milimani.

pia jini huyu huwatia watu hasara kwa kujifanya anataka UGANGA na anunuliwe vifaa vya uganga.
na akiwa ni mahaba utamgundua hivii
mtu hachoki kufanya mapenzi.nk

TIBA YAKE

tibazakissuna.blogspot.com
#chukua

#mafuta ya mchaichai

#mafuta ya figiri

#mafuta ya nyangumi

#mafuta ya ndimu
changanya kisha uwe unapakaa kwa siku 45,

DAWA YA KULA

  • MSUBIANI
  • MJAFARI
  • MWINGWA JINI
  • MJABARI
  • KAMUN AS WAD
tibazakissuna.blogspot.com
kisomo ni HARB.

siku tano hadi saba mfululizo.pia dawa ya kufuta chale ya wanga ni muhimu kwa mgonjwa.
tibazakissuna.blogspot.com

 

Ijumaa, 12 Desemba 2014

DAWA YA MWENYE KUWAHI KUMWAGA MANII WAKATI WA JIMAI

KUCHELEWESHA KUMWAGA MANII ( HERBAL FOR DELAYING EJACULATION )


kwa kweli hili jambo ni jambo ambalo ni muhimu sana kutatuliwa,
kwani kama litaachwa huwa na madhara makubwa sana ndani ya ndoa.
pia huweza kusababisha hali michepuko iwapo mke hapatiwi haki yake stahivu.
kwanini mtu ana wahi kufika mapema?

ina weza kutoka na sababu nyingi ikiwamo KAZI NGUMU ima kuinama zaidi na kuumiza mgongo au KUTANUA MAPAFU kwa kuinua vitu vizito.
na ukumbuke kuwa msafara wa manii huanzia baina ya mgongo na mbavu.

NJIA YA KUJITIBIA

chukua MAFUTA YA ZAITUNI kisha
tibazakissuna.blogspot.com
mafuta hayo ya ZAYTUNI changanya na MAFUTA YA NYONYO {mbono} au wengine huita mafuta ya mbarika.

VIPIMO

ZAYTUNI robo lita
 
MBONO  ml 25

kisha unakanda mgongo KATIKATI YA UTI wa mgongo mpaka KIUNONI.
kisha unapaka na maeneo ya UUME.

kila siku nusu saa kabla hujafanya JIMAI.
basi utakuwa ukiongeza muda wa kuchelewa mpaka utakapo fikia hatua ya kuona hapa PANATOSHA ndipo utaacha ili usije kuleta kero badala ya furaha.

tibazakissuna.blogspot.com

Alhamisi, 11 Desemba 2014

TIBA YA KUONDOA MVI KICHWANI


MVI ni nywele ambazo huota kichwani kwa mwanaadamu lakini zikiwa na rangi nyeupe badala ya nyeusi, na nywele hizo huitwa nywele zilizo chakaa,
na nywele hizo huwa ni chukizo kwa mwenyezo iwapo hajafika umri wa miaka 40.
na huangaika sana ili kuondoa mvi hizo.

JINSI YA KUJITIBU

chukua KITUNGUU SWAUMU , halafu
tibazakissuna.blogspot.com
Uwe unameza kama kidonge kwa maji BILA kukisaga, utameza VITATU kutwa mara tatu kwa muda wa miezi MITATU mfuatano mpaka MINNE,
mvi zitakuwa zimeondoka. bi idhni llaah

Jumatatu, 8 Desemba 2014



ASALAAM ALYKUM

KWA WALE WOTE WENYE MATATIZO YA KIAFYA NA MAJINI KWA SASA NIPO MKOA WA KILIMANJARO.

KWA WALIOPO KARIBU NA MOSHI NA WALIOPO MOSHI PIA NI MUDA WAKO SASA KUJA KUPIMWA KWA MASHINE NA KUPATA TIBA KWA NJIA YA KISSUNA
PIA UTAFANYIWA RUQYA NA VISOMO VINGINE VYA KUWAANGAMIZA MASHETANI WAKOROFI NA KUPATA DAWA ZA KUONDOSHA UCHAWI UNAO TESA AFYA ZETU WANADAMU.

PIA KWA WALE WENYE KUHITAJIA VITABU NA YALE MAFUTA

KWA MAWASILIANO

+255 753 549 090
+255 713 826 838
+255 655 826 838
+255 774 826 838
+255 655 826 838
+255 772 156 789
+255 784 638 989

ASSALLAM ALLYKUM

Jumamosi, 6 Desemba 2014

MAAMBUKIZI YA NJIA YA MKOJO ( U.T.I )



MAAMBUKIZI YA NJIA YA MKOJO ( U.T.I )


Maambukizi mengi ya njia ya mkojo hua yana shambulia kwenye kibofu cha mkojo (blader), 
ingawa hutibika kirahisi pindi unapo pata tiba mapema kama itakoma sana huenda ikashambulia figo (kidney) na ikiwa imefika kwenye figo hua ni tatizo kubwa.

mwili hua na tabia ya kujikinga wenyewe ( immune ) kwa kuua bacteria pia kuwasafisha bacteria nje  kwa kukojoa na kutoa haja kubwa hii hutoa vijidudu (microbes) vilivyo kufa na vilivyo hai kama taka .

Mwanamke hua ni mwenye kuathirika kwa wepesi zaid kwa kua njia yake ya MKOJO ipo karibu sana na sehemu ya HAJA KUBWA hivyo pindi mwanamke anapo jisafisha kwa kuleta MAJI MBELE hupelekea  kuleta bacteria Escherichia coli (E. coli) ambae huleta UTI kwenye tundu la mbele

 Hivyo hushauriwa kujisafisha  kwa kurudisha MAJI NYUMA kwa mkono wakati wa kujisafisha haja kubwa

DALILI ZA U.T.I

  • MAUMIVU YENYE KUCHOMA CHOMA PINDI UNAPO KOJOA


  • KUKOJOA MKOJO WA MANJANO AU WADAMU


  • KWA MTOTO MDOGO HUPATA HOMA KUSHINDWA KULA NA HULIA SANA


  • MAUMIVU YA UTI WA MGONGO NA CHINI YA KITOVU

TIBA YAKE 

© tibazakissuna.blogspot.com

WEKA KIJIKO KIMOJA CHA BAKING SODA KWENYE GLASS MOJA YA MAJI KISHA KUNYWA MARA MOJA KWA SIKU NDANI YA SIKU 7, HUKU UKIENDELEA KUNYWA MAJI YA KAWAIDA

KISHA CHUKUA MCHANGANYIKO WA ASALI NA UNGA WA MDALASINI CHANGANYA UTATUMIA KIJIKO KIMOJA KWA SIKU 7

NI BORA UKITUMIA DOZI ZOTE MBILI  KWA PAMOJA KWANI HUONDOA U.T.I SUGU

Alhamisi, 20 Novemba 2014

TATIZO LA KUKOSA HEDHI ( AMENORRHEA )





TATIZO LA KUKOSA HEDHI ( AMENORRHEA )


Kuto kupata hedhi kuna pelekea mawazo na mashaka kwa wanawake wengi pindi tatizo hili linapo jiri
Tatizo hili huweza kutokea 

Mapema Mwanzoni ( PRIMARY ) ambapo msichana hua katika umri wa kuvunja ungo (16) ila hapati mabadiliko ya kimaumbile yanayo ambatana na kuvunja ungo PIA anaweza kupata dalili zote za kuvunja ungo kama kuota nywele sehemu za siri na kuota matiti ila bado pia hapati hedhi

Pia linaweza kutokea 

Badae katika Maisha ( SECONDARY ) Ambapo mwanamke hayupo katika hali yoyote ya kumzuia kupata hedhi kama vile ujauzito, kunyonyesha au kutokuwepo katika kipindi cha Menopause yaani yupo chini ya miaka arobaini.

NININI HUSABABISHA KUTOKUPATA HEDHI

> Kupata Hitilafu katika viungo vinavyopelekea mwanamke kupata hedhi ambavyo ni matezi yake ya hypothalamus, pituitary, kizazi (uterus) na kiwanda cha kutengenezea mayai (ovaries)

> Madhara yanayo tokana na matibabu ya kansa

> { functional hypothalamic amenorrhoea } hii ni hali inayo kusanya sababu nyingi za kawaida ambazo ni
> Msongo wa Mawazo  Kupungua mwili  Kuzidisha kati ya kula au mazoezi na pia maradhi

> Kulogwa au Kua na Majini Mahaba

MATIBABU

© tibazakissuna.blogspot.com

Chukua dawa inayo itwa SUFA.
Iwe ya UNGA ujazo ni Robo kilo 

changanya na chumvi ya unga ujazo huo huo.  

Halafu awe anachota kijiko kimoja kidogo na kuweka katika Maziwa ya Moto kikombe kimoja.
Kila siku Asubuhi na Usiku. Mpaka amalize hiyo dawa. 


Lakini kama atakuwa na Jini Mahaba basi damu itafunguka 

http://tibazakissuna.blogspot.com/

Jumanne, 18 Novemba 2014

TATIZO LA KUZIBA KWA MIRIJA YA UZAZI ( Blocked fallopian tubes)




Mirija ya uzazi kwa mwanamke (fallopian tube) ni mirija miwili kila moja upande mmoja inayo unganisha  kati ya OVARIES (ambapo mayai huzalishwa) na mayai yanapo komaa hupitia sasa kwenye mirija ya fallopian na yai kukutana na mbegu za kiume na kua (fertilezed) na kushuka kwenye UTERUS (kizazi) kwa ajili ya uzalishaji 


AINA YA UZIBAJI WA MIRIJA 

Matatizo katika mfumo wa uzazi huanzia aidha ukeni au ndani ya kizazi. Maambukizi ya ukeni huweza kujipenyeza hadi ndani ya kizazi na kushambulia tabaka la ndani ya kizazi na mirija.

HYDROSALPINX  hii hua ni mirija ya yai kuongezeka kwa umbo kutokana na mirija kujaa maji na kuzuia mbegu kupita ili kukutana na yai na hali hii kupelekea kutokupata mimba


NINI HUPELEKEA KUZIBA KWA MIRIJA

> PID = (PELVIC INFLAMMATORY DISEASE) Hii hua ni matokeo ya maambukizo ya zinaa ambapo huleta makovu yenye uvimbe na kusabaisha mbegu kutopita, ila sio lazima uwe una ugua hata kama ulikua una historia ya kuugua mara kwa mara magonjwa ya zinaa kama kisonono hupelekea hali hiyo

> Historia ya kufanyiwa UPASUAJI wa sehemu zisizo za kawaida kama tumboni na kizazini

> ECTOPIC PREGNANCY kutunga mimba kwenye mirija ya uzazi ( fallopian tube ) na kutokushusha yai kwenye kizazi  ambapo huleta hatari zaid na hugundulika baada ya wiki nane kwa vipimo, pia yai huweza kutunga kwenye mdomo wa kizazi (cervic).

> Kufanyiwa upasuaji kwenye mirija ya uzazi ( fallopian tube )

> Kutoa Mimba

DALILI ZA KUKUJULISHA 

# Maumivu chini ya kitovu yasiyo kwisha 

# maumivu wakati wa jimai 

# Kutokupata ujauzito hata kama ulipata mara moja

# kutokwa na uchafu usio wa kawaida kwenye uke


TIBA

© tibazakissuna.blogspot.com

Chukua SANAMAKI na ZATTARI ujazo sawa.
 Kisha chota ujazo wa NGUMI yako uchemshe kwa MAJI LITA MOJA NA NUSU
Yachemke mpaka yabaki NUSU LITA halafu utakunywa ASUBUHI na USIKU
utakunywa kwa siku MOJA  tuu
 Kisha utarejea tena baada ya MWENZI MMOJA
LAKINI  kabla ya kuandaa upya UKAPIME kama hauna mimba ili kama utakuwa na mimba USINYWE

Jumatatu, 10 Novemba 2014

MAJINI AINA YA ZAWAABIL



MAJINI ZAWAABILI


Majini hawa husababisha maradhi yafananayo na ya kansa au mkanda wa jeshi.
Ni majini wapumbavu sana.
Na humuingia kwa wepesi mtu mwenye TABIA YA KUPENDA KUKAA WAZI MWILI WAKE AKITOKA KUOGA
Na akiwa ni JINI MAHABA aina hii hutopenda kusikia wala kukaa na mwenye kunuka jasho ila utakuwa mwenye kutema tema mate.


DALILI ZAKE


  • Mwili kuwasha sana
  • Ngozi kubabuka
  • Ngozi kuvuka kama gamba la nyoka
  • Mwili kuvimba na kuwaka moto
  • Mwili kuwa na midonda ya mapele

KUWAONDOA KWAKE

© tibazakissuna.blogspot.com

Kisomo cha KHAWAATIMU siku 11

Na dawa zakupakaa ni MRUTURUTU changanya na MAFUTA YA NYONYO au MAFUTA YA NDIMU pakaà siku 27
 

Dawa za kunywa ni MKUNAZI na SUFA NYEKUNDU siku 27
 

KWA MAWASILIANO ZAIDI YA TIBA NA KISOMO

+255 713 826838
+255 655 826838
+255 784 638989
 




Ijumaa, 31 Oktoba 2014

JINNI JADI





JINNI JADI 

ni aina ya majini ambayo huleta athari za kiafya na kimaendeleo katika mwili wa mwanadamu
ila utajuaje kua umeathirika na jini wa aina hii 

DALILI ZAKE
  • KULALA NA KUOTA UNAZIKWA
  • KUOTA MISIBA MARA KWA MARA
  • BABU AU BIBI MMOJA WAO ALIKUA MCHAWI NDO MAANA UNASUMBULIWA
  • WAGANGA WATASEMA KUA UNA MIZIMI YA KWENU INAKUSUMBUA
  • UNAKUA NA CHALE NDOGO NDOGO KWENYE USO AMBAPO HUWEZ KUPONA MPAKA CHALE HIZO ZA WACHAWI KUFUTWA NA KUMUONDOA HUYO JINI 
  • UKIWA MWENYEWE CHUMBANI UNA HISI KUNA MTU ANAKUFATA NA UNASKIA NYAYO ZIKIKUKARIBIA ILA HUONI MTU UNAPO GEUKA KUANGALIA
MADHARA YATOKANAYO NA JINI HUYO
  • Pesa kupotea katika mazingira ya ajabu [ chuma ulete ]
  •  kivuli chako kutumika kulogea 
  • Kua na asili ya uganga wa jadi
  • Kufanywa msukule 
 MSAADA WA HARAKA:

© tibazakissuna.blogspot.com

ANDIKA BISMILLAHI  RAHMAN RAHIM   بسم الله الرحمن الرحيم    MARA 35  
UWEKE CHINI YA MTO WAKATI WA KULALA ITATULIZA TATIZO ILA HUJATIBU TATIZO KUTIBU INABIDI UPATE TIBA. 


Jumanne, 21 Oktoba 2014

TIBA YA MINYOO (Ascariasis)




MINYOO 

hutokana na kunywa au kula chakula chenye mayai ya round worm.
pindi unapo kula mlo wenye mayai hayo basi yai hutamia na kutoa mayai machanga larvae,
Ndani ya siku kadhaa larvae hutembea kwenye kwenye njia za damu mpaka kwenye mapafu hapo huleta hali ya mapafu kubana na kuuma ( eosinophilic pneumonia ),
Hurudi kwenye utumbo mpana na kuendeleza mazalia na kukomaa na kuishi ndani ya mienzi 10 mpaka 24.

DALILI ZA MINYOO 


  • kupata choo chenye minyoo
  • kutapika minyoo
  • kukohoa damu 
  • kupata pumzi kwa tabu kutokana na mbavu kubana 
  • kupata kizunguzungu kutokana na kupungukiwa na damu
  • tumbo kujaa na kuisi gesi nyingi

TIBA KWA MINYOO

© tibazakissuna.blogspot.com

Chukua VITUNGUU SWAUMU kisha saga juice.
Upate ujazo wa robo Lita
Kisha saga SHUBIRI kijiko kimoja cha chakula
Halafu weka na ASALI vijiko 3 vikubwa.
Kisha unakunywa ujazo wa kikombe cha kahawa kutwa Mara tatu.

Utafanya kwa siku 5.

Jumamosi, 18 Oktoba 2014

TIBA KWA MATATIZO YA MACHO

 


MAUMIVU YA MACHO 

Yako magonjwa ya aina nyingi ya matatizo ya macho kutegemeana na chanzo cha tatizo.
japo ntagusia kuhusu matatizo mengine ya macho ila ntaongelea zaidi JICHO KUCHOMA CHOMA NA KUPELEKEA MAUMIVU

SABABU YA TATIZO
  • Kuangalia sana tv,simu au kompyuta
  • Kusoma kwa muda mrefu
  • Ukosefu wa usingizi
  • kutumia vikuza muonekano (lenses)

TIBA YAKE

© tibazakissuna.blogspot.com

> Tumia MAJI YA BARIDI kuoshea uso

> Tumia ROSE WATER kusafishia jicho kwa kuweka kwenye pamba ukikosa tumia matone ya SHUBIRI 

> ASALI na MAJI changanya kwa ujazo sawa kisha pakaa kwenye jicho likiwa lime jifunga

> Kata kipande kidogo cha TANGO kisha weka kwenye jichoukiwa umelifunga ukiwa umejilaza chali  kwa dakika 15

> Unaweza kukosa vyote sio mbaya pia kama utafunga jicho na kujiweka kijiko juu yake kwani ubaridi wake huleta nafuu

MATATIZO MENGINE YA JICHO 

 > JICHO LILILO VIMBA NA KUA JEUSI KANDA KWA BARAFU NDANI YA DAKIKA KUMI NA TANO AU 20 KILA SIKU

JICHO LINALO UMA KUTOKANA NA SABUNI BASI MIMINIA MAJI YATIRIRIKIE KWENYE JICHO NA KUSHUKA CHINI

> KWA JICHO LILOKUA KAVU CHUKUA KITAMBAA CHA MAJI YA MOTO KISHA KANDA JICHO

> KWA JICHO LILIO INGILIWA NA PILIPILI BASI WEKA MAZIWA KWENYE KIKOMBE KISHA FUNGUA JICHO MAZIWA YAINGIE KWENYE JICHO UKIKOSA CHANGANYA CHUMVI NA MAJI KISHA SAFISHIA JICHO KWA MAJI HAYO

> KWA VIJIPU MBUZI VILIVYO KWENYE JICHO OSHEA USO KWA MAJI YA CHUMVI YENYE VUGU VUGU

TIBA KWA KUPITIA VYAKULA

  • KUNYWA JUISI YA KAROTI KWA WINGI

  • KULA VYAKULA VYA ASILI YA KIJANI

  • KULA SAANA MBEGU ZA ALIZETI


Alhamisi, 16 Oktoba 2014

TIBA KWA ANAE POTEZA KUMBUKUMBU


KUPOTEZA KUMBUKUMBU


Ni uwezo mdogo wa kuhifadhi kumbukumbu kwa ajili ya matumiz ya akili.
Kuna kupoteza kumbukumbu ya jambo lililo tokea siku nyingi (long term memory) au jambo ambalo halijapita hata sekunde thelathini ukawa umelisahau (short term memory)

SABABU HUA

> UZEE

> MADAWA YA PRESSURE AU MADAWA YA MAUMIVU

> AJALI ZILIZO ATHIRI SEHEMU ZA UBONGO 


TIBA YAKE  

© tibazakissuna.blogspot.com

chukua ROSE zile  tunda zake. zilivyo zipo kama KOROSHO zilizo banguliwa.
kisha awe anatafuna 21 asubuhi na usiku baada ya kula  kwa muda wa mwenzi mzima 30 siku.
kupaka kichwan ataondoa nywele kichwani kwanza awe UPARA kisha tumia MAFUTA YA ROSE na ZAYTUNI akiwa anatafuna tunda hizi ale mbegu hizi basi anakua anapakaa kichwan hayo mafuta yatasaidia

1 )  kuimarisha mishipa ya ubongo 

2 )  kurejesha kumbukumbu 

3 )  kuongeza fahamu na akili

4 )  kujenga ubongo 

Jumatano, 8 Oktoba 2014

UPUNGUFU WA DAMU MWILINI (ANEMIA)





UPUNGUFU WA DAMU MWILINI 

ni ugonjwa unaosababishwa na upungufu wa seli hai nyekundu kwenye damu pia huweza kua na maana ya pili ambayo ni tatizo la damu kushindwa kubeba oxygen.

SABABU ZA UPUNGUFU WA DAMU

1)  Kupoteza damu kwa wingi kutokana na majeraha au magonjwa yanayo pelekea kuvuja damu
2)  kuzidi mvunjiko wa seli nyekundu kwenye damu

DALILI

> Kujihisi  kuchoka

> Kua mdhaifu na kupoteza umakini kwa jambo unalo shughulikia

> kupoteza pumzi

> kupata kizunguzungu au kuzimia mara kwa mara

* Vyema kupima kwani dalili hizi hushabihiana na magonjwa mengine

TIBA YAKE

>  Tafuta ASALI YA TENDE ml 250
Chemsha pamoja na MAUA DAMU ( karkadee) ikichemka tayari
Chukuwa ujazo wa kikombe cha robo lita ikiwa na uvugu vugu uweke ROSE MARASHI kijiko kidogo cha chai.

Kisha anywe.
Atatumia kutwa mara tatu kwa siku 27
Atapona kabisa in shaa Allah


 

Jumamosi, 27 Septemba 2014

MAJINI AINA YA SWAARIU


MAJINI AINA YA SWAARIU 


Majini wa Swaariu pindi wakishirikiana na wachawi basi huweza kukusababishia uchawi aina ya NAAFITH ambao umetajwa katika
QURAN > "JILINDE KUTOKANA NA UCHAWI UNAPO PULIZA KATIKA MAFUNDO YALIYO FUNGWA"

Uchawi huo wa NAAFITH unapoletwa mwilini huchokuliwa miti ya hanjari na fayja kisha huchanganywa na mafuta ya mtoto aliekufa wanaweka kwenye QABBU ambayo ni mfano wachupa ndogo huku wakisema maneno yao yakichawi,kisha inakwenda kwa mfano wa upepo na kumvaa muhusika na mtu huanza kuumwa.na uchawi huo wa majini aina ya SWAARIU hua unatulia katika moyo na kuleta presha ya kupanda na kushuka na ukipima hospitalini huoni ugonjwa.

TIBA YAKE:

Majini hawa ili uwatoe kwanza mgonjwa asomewe RUQYAT,

DAWA ZA KULA

>  KAMUUN AS-WAD

>  SUFA

>  MJAAFAR

Dawa hizo utachanganya kwa ujazo sawa na kisha awe ananywea kwenye uji siku 19.

Pia apate MAFUTA ya

>  ZAITUNI 

>  NDIMU 

>  NYONYO

Achanganye mafuta yote kwa ujazo sawa na apake kwa siku 19


Ijumaa, 26 Septemba 2014

TIBA YA M`BA



UGONJWA WA M`BA NA MATIBABU YAKE


 M`BA ni ugonjwa wa ngozi ambao hushambulia sehemu ya kichwa, Hii hutokana na kuwepo kwa bacteria na fangasi katika ngozi ambapo hupelekea ngozi kuwasha na kuwa kavu. HUU ugonjwa hukumba watu warika zote na huonyesha makali saana wakati wa baridi na mvua.

SABABU YA TATIZO

Kitaalamu haijajulikana mpaka sasa nini huleta M`ba kichwani ila kwa tahadhari ni vyema kukausha maji pindi yanapo kua kichwani kutokana na kuoga au mvua usiache maji yakaukie kichwani na pia epuka vumbi jingi kwa kuosha vumbi pindi linapo fika kwa wingi kichwani.

MATIBABU

MAFUTA YA ZAITUNI > Chukua mafuta ya Zaituni chemsha yapate joto kisha pakaa kichwani kwa kusugulia kichwani kisha utafunika kichwa kwa muda wa lisaa limoja baada ya hapo utachukua brashi kutoa m`ba na utaosha kichwa kwa maji ya baridi.USISAHAU KUKAUSHA KICHWA 

LIMAO > Chukua vijiko viwili vya juice ya limao utasugulia kichwani na kusubiria kwa dakika 3. utachukua kikombe kidogo chenye maji na utaweka juice ya limao kijiko kimoja utaoshea kichwa mchanganyiko ho na kukausha kichwa na taulo safi utafanya hili zoez kila siku mpaka m`ba ziishe


VITUNGUU SWAUMU > Menya vitunguu swaumu kisha saga vitunguu swaumu, kisha weka msago huo kichwan kwa muda wa nusu saa kisha utatoa na kuosha kichwa kwa maji ya barid na ukumbuke kukausha maji.
DAWA hii kwa MTOTO NA MWENYE ALLERGI  itabidi uwekee maji kidogo kuepusha maumivu makali kwa ukali wa dawa




Jumatano, 17 Septemba 2014

TIBA KUPITIA ASALI NA MDALASINI





FAIDA ZA MCHANGANYIKO WA ASALI NA MDALASINI

Matatizo mengi yanayosumbua jamii hutibika sio tu kwa hospitali bali meng hutibiwa kwa njia za asilia haswa za kissuna. Tuangalie faida za Mdalasini na Asali kwa baadhi ya maradhi

1)  MATATIZO YA KIBOFU > vijiko viwili vya unga wa mdalasini na vijiko viwili vya asali changanya vyote na glass moja ya maji ya moto  tumia asubuh na usiku 

© tibazakissuna.blogspot.com



2)  KANSA  >  Utapata matukeo mazur kwa kansa ya mifupa na tumbo,chukua kijiko cha asali na kijiko cha mdalasini changanya kisha tumia mara tatu kwa siku muda wa mwenzi mzima

3)  MATATIZO YA UZAZI  > Kwa mwanaume tumia vijiko viwili vya asali kila unapo kwenda kulala itakupa manii zenye uimara 
  kwa mwanamkechanganya mdalasini na asali zote nusu kijiko kisha finya mchanganyiko huo kwa vidole na uweke kwenye fizi za meno ili ujichanganye na mate uingie mwilini na kuimarisha mfuko wa uzazi

© tibazakissuna.blogspot.com

4)   TUMBO  > Asali na mdalasini huondoa maumivu ya tumbo,huondoa gesi na hutibu vidonda vya tumbo kwa kuondoa wadudu walioko tumboni na pia kukupa afya nzuri.

5)  MAFUA >  Wanasayansi wa spain wamethibitisha kua asali hua na mchanganyiko ambao huasidia kutibu mafua

6) MAGONJWA YA NGOZI  >  Pakaa asali na mdalasini kwa makadirio sawa hutibu magonjwa yote ya ngozi 

7) HARUFU MBAYA YA KINYWA >  kitu cha kwanza asubuhi piga mswaki kwa mchanganyiko wa asali na mdalasini kijiko kimoja kwa kila dawa kisha sukutua kwa maji moto

8) PUNGUZA UNENE  >  
                                         NJIA YA KWANZA
 tumia kwa mfumo huu  yaani asali iwe nyingi kuliko mdalasini mfano kijiko kimoja cha mdalasini kwa vijiko viwili vya asali 

                                         NJIA YA PILI
chemsha kikombe kikubwa cha maji kisha epua maji weka mdalasini acha yapoe kwa nusu saa na hakikisha maji yamepoa ndo uweke asali kwan maji yamoto huua virutubisho vya asali kisha utakunywa NUSU ya mchanganyiko huo usiku wakati wa kulala kisha asubuhi malizia mchanganyiko huo BILA kuuchemsha tena

9)  CHUNUSI  > chukuavijiko vitatu vya asali na kijiko kimoja cha mdalasini kisha weka mchanganyiko huo kwenye chunusi kabla hujalala kisha asubuhi utautoa kwa maji ya moto tumia kila siku ndani ya wiki mbili chunusi zitakwisha

© tibazakissuna.blogspot.com

FAIDA ZINGINE > huongeza nguvu na kukupa uchangamfu pia huongeza nguvu za kiume na kukusaidia kujiskia vyema katika tendo, hurudisha nywele, kwa vipara huongeza nguvu za mwili na kukusaidia kuto kuzeeka mapema, na ndio tiba pekee inayotibu magonjwa ya mifupa
(Arthritis).


© tibazakissuna.blogspot.com

Jumatatu, 15 Septemba 2014

KUTOKUZALISHA KWA MWANAUME (male infertility)

KUTOKUZALISHA KWA MWANAUME 

 Ni tatizo ambalo huwakumba Wanaume wachache japo ukuwaji watatizo hili ni wakasi 

SABABU ZIKIWA NI

1)TATIZO LA UZALISHAJI WA MBEGU (Sperm Production Problem)  >  hili ni tatizo kubwa miongon mwa yote ambapo uzalishwaji wa manii hua ni mchache au manii kua dhaifu na kutokuweza kufanya kazi ipasavyo

2) VIZUIZI KWENYE MIRIJA (Blockage of Sperm Transport)  >  vizuizi kwenye mirija inayopeleka manii kwenye dhakari na kusababisha manii kutokutoka ipasvyo au kutokutoka kabisa

3) NGUVU ZA KIUME  >  japo sio tatizo kubwa lakini pia kutokuweza kusimamisha ipasavyo au kutoweza kujihimili na kumwaga mapema kabla ya kumuingilia mwanamke ndani ya uke  hua ni tatizo

4) HOMONI  >  Saa zingine  tezi (pituitary gland) hazitoi taarifa sahihi za homoni kwenye makende hili tatizo hupelekea uzalishwaji mdogo wa manii au kutokuzalishwa kabisa

MAZINGATIO KABLA YA DAWA

Acha Uvutaji SIGARA kama unavuta maana hupunguza kasi ya uzalishaji wa mbegu

Epuka JOTO jingi kwenye sehemu za uume maana huua ubora wa manii zilizo zalishwa kwa muda huo Allah mjuzi zaidi anajua kwanii kiungo dhakari na makende vimewekwa njee

TIBA

Chukua RAWANDI kisha yeyusha kwa maji ya DAFU au maji ya NAZI  halafu kunywa mara MBILI kwa siku ndani ya siku TATU
BAADA YA KUMALIZA HIZO SIKU TATU kata KABICHI ziwe ndogo ndogo saana weka KARANGA MBICHI kisha mwagia ASALI alafu utafune mchanganyiko huo kwa kipimo cha MKONO wako 
utatumia siku SABA ukiwa unaandaa kila siku na kutumia mara moja kwa siku mpaka siku saba
utapata mbegu za KASI na UHAI