Ijumaa, 21 Agosti 2015

KUANGUKA SHULENI





KUANGUKA KWA WANAFUNZI SHULENI

tunapo ongelea sababu za maradhi ya kuanguka mashuleni basi tunaweza kuongelea janga la Kitaifa.

 na ndiyo maana pindi linapotokea janga hili huhitajika sana viongozi wa dini ili kuleta msaada. lakini kama ilivyo kawaida huwa kila kitu kina fani na mwenye fani. tatizo hili la kuanguka huambatana pia tatizo mwenza ambalo ni tatizo la kucheke cheka kwa watoto wa kike. Tanzania tatizo hili limewahi tokea Tabora girls na Mbeya Girls. lakini nini chanzo?
 chanzo cha tatizo hili ni 

1) KUJENGWA SHULE KATIKA UWANJA WA WACHAWI
 

2) KUJENGA KATIKA NGOME YA MAJINI

3).KUJENGA KATIKA MSAFARA WA MAJINI

© tibazakissuna.blogspot.com

sasa utajuaje sehemu iliyo au inayokaliwa na vikao na wachawi??
Wachawi huwa vikao vyao hukaa katika miti aina ya
 

1} MKUNGU

2} MKOROSHO

na ikiwa mji hauna miti hiii basi huangaliwa mti mkubwa ambao umefikia miaka 12 na zaidi mpaka 30
kisha hukalia vikao vyao mfano wa muembe nk.

hivyo ujenzi wa shule ukifanywa basi watoto watakuwa wanakutana na vitu vya ajabu na maradhi ya kushangaza yenye kushtukiza. na kama itakatwa kabla ya ujenzi basi watoto au walimu watakaa kwa shida na akili kuwa kama watu ambao si timamu iwapo hapakufanywa dua ya KUSWARIFU AMMAAR.

 
© tibazakissuna.blogspot.com 

Majini wana maeneo yao ambayo wanaishi kama vile baharini au mito na milimani au visimani na jangwani au chooni nk.
lakini elewa kuwa miongoni mwa maeneo wanayoishi ni katika miti kama 


Mibuyu 

Misufi 


Mikuyu


Mikenge


nk
na miti hii hupendwa sana mashuleni. sasa basi iwapo shule imejengwa hali miti ilikatwa jua kwamba wanafunzi wengi watapatwa tatizo la ugonjwa wa macho au vichwa na kupelekea kuvaa miwani ya macho.
na kama haiku katwa basi watakuwa na tatizo la kuanguka.

pia kuna kujenga katika njia ya majini.

ambapo huwa ni majengo yanayo kuwa maeneo ya jangwani huwa na mfumo wa upepo usio vuma na hewa nyepesi kama upepo wa bahari. maeneo hayo yakijengwa pia hupelekea watoto na walimu kuanguka au kucheka cheka hovyo.


 pia husababisha kupatwa na majini mahaba aina ya Bedui Biduan
ambapo madhara hupelekea watu kuwa na pepo la ngono
mtu anawaza ngono bila kuwaza lolote na ndiyo sababi zipo shule zina sifika kwa ukahaba hali yakuwa watoto walipelekwa wakiwa ni wenye maarifa na maadili

  
 © tibazakissuna.blogspot.com
 

NINI KIFANYIKE

kabla ya kujenga jengo basi ilitakiwa pasomwe suurat yaasin 21
kisha upatikane 


A} msaka uchawi


A} mdaula


A} mkunazi


yote iwe majani na kisha ilowekwe katika maji na kumwaga eneo la shule tarajiwa.
na kama imekwisha jengwa tayari
hapo panatakiwa ufundi wa kutosha. kwa sababu inatakiwa kwanza ipatikane zaytshifaa
kisha iwekwe katika maji yamwagwe katika madarasa yote na watoto na walimu wakae uwanjani wafanyiwe visomo vya harbu l qatl au Sayf l qatw ii. ambavyo huwa ni visomo vigomo sana kwa sababu hubadilika kutokana na visomo vinavyo kwenda na aina ya majini watakao panda kwa wagonjwa husika.


DAWA ZA KULA


B} msigi

B} mfuleta


B} mvuma nyuki


B} mfa usiku


B} mrehani


B} kamun as wad

kisha 


apakae zayt shifaa
siku 90
in shaa Allah watapona.
tibazakissuna.blogspot.com

0 maoni:

Chapisha Maoni